Ticker

10/recent/ticker-posts

Aisee...!!!! Mlinzi Takukuru aua mchumba baada kukataliwa ndoa


Alikuwa amemsomesha unesi,alipomaliza kusoma akasema sitaki tena ndoa,nimepata mchumba mwingine

Taarifa ya RPC mkoa wa Ruvuma
BEATA Kafuru mkazi wa Mtaa wa NHC, Tunduru Mkoani Ruvuma, mwenye umri wa miaka 26 amefariki kwa kinachodaiwa amepigwa risasi 3 kichwani na Mchumba wake James Paul(27) mlinzi wa TAKUKURU na kufariki papohapo ndani ya nyumba wanayoishi, chanzo kinadaiwa kuwa ni wivu wa kimapenzi.

Marehemu alikuwa Muuguzi Hospitali ya Wilaya Tunduru na ameacha Mtoto mchanga wa miezi 11 aitwae Aviera, mtuhumiwa anasema wameishi pamoja kwa miaka 4 hadi wakazaa na walipanga kuoana, Beata akaenda kujiendeleza kimasomo Peramiho aliporudi akabadilika na kudai hamtaki.

Kwahiyo chanzo ni wivu wa kimapenzi na kulipiza kisasi kwasababu James anadai marehemu alikuwa anamtamkia Waziwazi kwamba hamtaki wakati alikuwa anampenda sana na hakuwa tayari kushare na mwingine, ila Binti kasema amepata mwingine na akataka waachane.

Kabla ya tukio mtuhumiwa alikuwa lindoni Ofisi za TAKUKURU na akatoka lindoni kwenda kutimiza adhima yake, James alipoua akataka kujiua pia, lakini kumbe risasi zilikuwa zimedondoka Housegirl akamuwahi kwa kupiga kelele Askari waliokuwa Doria wakafika.

Katika eneo la tukio tumekuta Pistol aina ya Browing (mali ya TAKUKURU), risasi nne ambazo hazikutumika na maganda matatu ya risasi, James tunamshikilia na tutamfikisha Mahakamani, mwili wa marehemu umehifadhiwa katika chumba cha maiti Hospitali ya Wilaya Tunduru...
Toka kurasa wa Benjamin Kasenyenda Andongolile.....


from MICHUZI BLOG https://ift.tt/32zyUVu
via

Post a Comment

0 Comments