Ticker

10/recent/ticker-posts

HALMASHAURI YA JIJI LA TANGA YAENDELEA KUWA KINARA UTOAJI WA MIKOPO ASILIMIA 10 -RC SHIGELLA

MKUU wa Mkoa wa Tanga Martine Shigella akiwasha pikipiki wakati kabla ya kuwakabidhi kundi cha vijana wa bodaboda cha Tanga One Youth.
MKUU wa Mkoa wa Tanga Martine Shigella akizungumza wakati wa halfa hiyo
MKURUGENZI wa Jiji la Tanga Daudi Mayeji akizungumza
MKUU wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa kulia akiwa na Mstahili Meya wa Jiji la Tanga Mustapha Selebosi wakiteta jambo wakati wa ziara hiyo
RTO wa Mkoa wa Tanga Solomon Mwangamilo kushoto akiwa na na Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga Leons Rwegasira wakijitambulisha kwenye mkutano wa hadhara wa mkuu wa mkoa wa Tanga Martine Shigella
Vijana wa kikundi cha Tanga One Youth wakiwa kwenye pikipiki zao wakimsikiliza mkuu wa Mkoa wa Tanga Martine Shigella baada ta kukabidhiwa
Sehemu ya wananchi wakimsikili za Mkuu wa Mkoa wa Tanga Martine Shigella



MKUU wa Mkoa wa Tanga Martine Shigella amesema kwamba Halmashauri ya Jiji la Tanga imeendelea kuwa kinara katika utaoji wa mikopo asilimia 10 kwa vikundi vya vijana, wakina mama na watu wenye ulemavu.

RC Shigella aliyasema hayo wakati wa ziara yake ya kutembelea wilaya ya Tanga iliyokwenda sambamba na kukabidhi mikopo ya pikipiki 70 kwa kikundi cha vijana cha Tanga One Youth.

Huku akieleza pia na vyarahani vya kutosha ya zaidi ya milioni 100 wamekopeshwa kila kata na watu wenye ulemavu nao pia wamenufaika navyo .

Alisema mikopo hiyo imekuwa chachu kubwa kwa makundi hayo na hivyo kuchochea kasi ya ukuaji wa uchumi wao na jamii zinazowazunguka ikiwemo kujikwamua kimaendeleo.

“Kwa kweli ninayofurahi kuona Tanga Jiji mmeendelea kuwa kinara kwenye utoaji mikopo asilimia 10 kwa mkoa huu wa Tanga lakini niwaambie watu walionufaika nayo kuitumia vizuri mikopo hiyo iweze kurejeshwa halmashauri na watu wengine waweze kukopa kwani haina riba “Alisema

Mkuu huyo wa mkoa aliwataka vijana watumie vizuri pikipiki hizo ikiwemo kuendesha kwa umakini huku akisema amefariji kuona RTO yupo eneo hilo huku akieleza kwamba hatarajii kusikia watu wanaondoa exosi na kuweka mfumo mwengine ambao unapiga kelele.

Awali akitoa taarifa ya mradi wa bodaboda kwenye kikundi cha vijana cha Tanga One Youth Afisa Maendeleo Jamii wea Jiji nla Tanga Dorah Ntumbo alisema kwamba halmashauri hiyo inatekeleza agizo la serikali la kutenga asilimia 10 ya mapato yake ya ndani kwa ajili ya utoaji wa mikopo kwa vuikundi vya wanawake,vijana na watu wenye ulemavu.

Alisema kwamba kwa mwaka 2018/2019 Halmashuri hiyo ilitenga jumla ya sh.milioni 800.449,700 kwa ajili ya makundi hayo ambapo vijana walitengewa jumla y ash.335,094,000 na hadi kufikia June 29 jumla ya Tsh milioni 353,000,000 zimekwisha kutolewa kwa ujumla wa vikundi 20 vya vijana.


from MICHUZI BLOG https://ift.tt/2ZTzCL3
via

Post a Comment

0 Comments