Ticker

10/recent/ticker-posts

WANA CCM SINGIDA MASHARIKI WAOMBWA KUSHIRIKIANA NA KUWA WAMOJA

Mbunge wa Jimbo la Singida Magharibi, Eribariki Kingu (kulia),akimkabidhi funguo ya pikipiki Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Wilaya ya Ikungi mkoani Singida, Mika Likapakapa aliyotoa kwa Wana CCM wa Kata ya Siuyu baada ya kumchagua Mbunge na Diwani kupitia chama hicho katika mkutano uliofanyika hivi karibuni wilayani humo. Kushoto ni Diwani wa kata hiyo, Selestine Yunde.
Ofisa Mtendaji Kata wa Siuyu, Bakari Kaduguda, akiwatambulisha viongozi wa kata hiyo kwenye mkutano huo.
Katibu wa CCM Kata ya Siuyu, Tito Lissu, akizungumza kwenye mkutano huo.
Mwenyekiti wa CCM Kata ya Siuyu, Yasin Dao, akizungumza kwenye mkutano huo.
Katibu Muenezi na Itikadi wa CCM Wilaya ya Ikungi, Pius Sanga, akizungumza kwenye mkutano huo.
Diwani wa Kata ya Siuyu, Selestine Yunde akizungumza na Wana CCM wa Kata hiyo katika mkutano wa kuwapongeza baada ya kuchaguliwa kuongoza kata hiyo uliofanyika hivi karibuni.
Wataalamu wa Kata ya Siuyu wakiwa kwenye mkutano huo.
Mkutano ukiendelea
Makofi yakipigwa kwenye mkutano huo.
Katibu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Wilaya ya Ikungi mkoani Singida, Noverty Kibaji akizungumza na Wana CCM wa Kata ya Siuyu katika mkutano wa kuwapongeza baada ya kumchagua mbunge na diwani kupitia chama hicho uliofanyika katika kata hiyo hivi karibuni.
Usikivu kwenye mkutano huo.
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Wilaya ya Ikungi mkoani Singida, Mika Likapakapa (kulia), akimkabidhi funguo ya pikipiki iliyonunuliwa na Mbunge Kingu, Katibu wa CCM Kata ya Siuyu, Tito Lissu.
Hapa ni wimbo wa CCM inachachamaa chaaa ukiimbwa 
Mbunge Kingu akiwa na Diwani wa Kata hiyo
Mbunge Kingu akizungumza.
Mkutano ukiendelea
Mkutano ukiendelea
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Wilaya ya Ikungi mkoani Singida, Mika Likapakapa akizungumza na Wana CCM wa Kata ya Siuyu katika mkutano wa kuwapongeza baada ya kumchagua mbunge na diwani kupitia chama hicho uliofanyika katika kata hiyo hivi karibuni.
Mmoja wa mwana chama aliyehamia CCM kutoka Chadema akila kiapo.



Na Dotto Mwaibale, Singida

WANACHAMA wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wa Singida Mashariki wameombwa kuwa pamoja na kushirikiana ili kuliletea maendeleo jimbo hilo.

Ombi hilo limetolewa hivi karibuni na Mwenyekiti wa CCM wa Wilaya ya Ikungi, Mika Likapakapa wakati akizungumza na Wana CCM wa Kata ya Siuyu katika mkutano wa kuwapongeza baada ya kumchagua mbunge na diwani kupitia chama hicho. 

"Nawaombeni wana CCM wenzangu wa Singida Mashariki tuwe kitu kimoja ili tuliletee maendeleo jimbo letu la Singida Magharibi ambayo yalichelewa kwa muda mrefu ukilinganisha na jimbo la wenzetu la Singida Magharibi linaloongozwa na Elibariki Kingu" alisema Likapakapa.

Alisema hivi sasa kata hiyo inaongozwa na viongozi kutoka CCM kuanzia Rais, Mbunge na Diwani hivyo wanakila sababu ya kupata maendeleo kwa kuwa tayari wanamafiga matatu na lugha itakuwa moja.

Katika mkutano huo Kingu alipata nafasi ya kukabidhi pikipiki yenye thamani ya sh.milioni 2 .2 aliyoinunua ikiwa ni zawadi kwa kata hiyo kufuatia ushindi mkubwa walioupata wa kumchagua Mbunge Miraji Mtaturu na Diwani Selestine Yunde wote kutoka CCM.

"Pikipiki hii ninayo wakabidhi niahadi yangu niliyoitoa wakati wa kampeni za uchaguzi mdogo wa diwani kuwa tukipata ushindi nitainunua ili itumike kwa shughuli za chama katika kata hii" alisema Kingu.

Katibu wa CCM wa wilaya hiyo, Noverty Kibaji alisema ushindi walioupata wa kumpata mbunge na diwani huyo ulitokana na maombi yao kwa mungu.

Kibaji alitumia mkutano huo kumshukuru Kingu kwa msaada wa pikipiki hiyo na kuwaomba wana CCM wa Kata hiyo kuitunza na itumike kwa kazi za chama na si vinginevyo.

Diwani wa Kata hiyo, Selestine Yunde alisema sasa anaanza kazi rasmi ya kuwatumikia wananchi na jambo atakalo anza nalo ni kushughulikia suala la mashine za kukusanyia ushuru ambazo zinalalamikiwa kutumika vibaya na kusababisha Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi na kata hiyo ya Siuyu ambayo ni sura ya wilaya hiyo kupata mapato kiduchu.


from MICHUZI BLOG https://ift.tt/33sfSS1
via

Post a Comment

0 Comments