Ticker

10/recent/ticker-posts

Ronaldo achangia bilioni 9.6 kwa Familia za Wachezaji Waliofia Katika Ajali ya Ndege


Bado dunia na ulimwengu wa soka kwa sasa unaomboleza msiba wa msafara wa timu yaChapocoense ya Brazil uliyopata ajali wakati wakielekea kutua uwanja wa ndege waMedellin Colombia.

Ajali hiyo ya ndege imehusisha watu 81 kati ya hao 76 wamepoteza maisha huku 72 kati ya hao walikuwa ni sehemu ya msafara wa timu hiyo na wachezaji wakielekea kucheza mchezo wao wa fainali ya kwanza ya Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Atletico Nacional ya Colombia.

Cristiano Ronaldo ni mmoja kati ya mastaa wa soka walioguswa kwa kiasi kikubwa na msiba huu, Ronaldo ameamua kuchangia euro milioni 3 ambazo ni zaidi ya Tsh bilioni 9.6 kwa timu yaChipacoense na familia za wachezaji wa timu hiyo waliyopoteza maisha