Ticker

10/recent/ticker-posts

Mwanamke aliyefanya mapenzi na Samaki atoa ya moyoni..Msikie hapa akifungiuka

Unaweza kushangaa na kuona ni kitu cha ajabu lakini hii imetokea ambapo mwanamke ambaye alifanya mapenzi na samaki aina ya Dolphin ikiwa ni sehemu ya utafiti wa kisayansi amezungumza kwa mara ya kwanza juu ya hatua hiyo.
Mwanamke huyo Margaret Howe Lovatt ambaye ni mtafiti wa wanyama amesema alikuwa sehemu ya utafiti huo uliofanyika katika kisiwa cha Virgin nchini Marekani kwa ajili ya kuwafundisha viumbe wa baharini wenye akili jinsi ya kuongea kiingereza.
Margaret Lovatt Howe
Margaret Howe Lovatt anasema alikuwa akijaribu kumfundisha Peter (the dolphin) jinsi ya kuongea kiingereza lakini uhusiano wao ulikwenda mbali zaidi.
Ilikuwa mnano wa mwaka 1963 ambapo walimsaidia kutengeneza bwawa la Dolphin nyumbani kwake ambako wanasayansi wangeweza kuwasoma wanyama hao wakiwa nyumbani, ndipo hapo Margaret alipokuna na Peter ambaye ni samaki aina ya Dolphin kwa wakati huo akiwa bado mdogo ambapo wawili hao wakapatana na mahusiano yao kukua zaidi kimwili.

Margaret amenukuliwa akisema kuwa “Peter (Dolphin) alipenda kuwa na mimi, mara nyingi alikuwa akijisogeza mwenyewe karibu yangu kwenye mguu wangu au mkono na kuruhusu kitendo hicho.”Anaendelea kusema kuwa “Haikuwa shida kwangu kwani Peter alikuwa akihisi uwepo wangu na kuona ni kitendo cha kimapenzi kwa upande wake lakini kwangu niliona ni kitu cha kawaida kama sehemu ya masomo yangu.”