Ticker

10/recent/ticker-posts

Udhaifu Huu wa Ali Kiba Unamfanya Diamond Ang'are

Ni ukweli usiopingika wasanii Diamond na Alikiba ni lulu ya taifa kwa sasa hasa unapozungumzia suala la usambazaji wa muziki wa Bongo Fleva kwenda zaidi kimataifa na kuufanya uwe na thamani hata kwa wasanii wengine watakapofikia level zao.

Leo nazungumzia utofauti mkubwa wa wasanii hawa wawili ambao mimi kama #KÄ°JANAMZALENDO nimeuona, Alikiba anaimba vizuri kuliko Diamond lakini kupitia kigezo cha kuimba pekee hakiwezi kumfanya kuwa Msanii mzuri kuliko wengine but kuna mambo mbalimbali ambayo msanii yeyote anapaswa kuyafanya ili awe bora zaidi kuliko wenzake.

1 Alikiba amekuwa akiamini yeye binafsi anaweza kufika international bila kufanya kazi na wasanii wa nje ya nchi Jambo ambalo Si la kweli ili Msanii yeyote uweze kufanikiwa kimataifa lazima ufanye Collabo na wasanii wa level hiyo mfano Wizkid sasa Dunia inamjua kupitia Drake, Davido dunia inamfahamu kupitia Meek Mill,

2 kufanya media tour na Show za kimataifa; Miongoni mwa mambo ambayo Alikiba yanamfanya awe tofauti na Diamond, Alikiba hafanyi media tour za nje anafanya za ndani tu Ndani kila mtu anaufahamu uwezo wake so tunataka aupeleke nje ya Tz pia aanze kufanya matamasha ya kimataifa haiwezekani msanii unataka kwenda kimataifa halafu kwa mwaka Unaperfom Majukwaa matatu tu.

3 Kupunguza Collabo na wasanii wa kawaida; kitu kingine ambacho Kiba anapaswa kukizingatia ni kupunguza Collabo haÅŸa wa wasanii wa kawaida ambao wanataka kupata jina kupitia yeye simaanishi kwamba asikuze vipajj lakini anaweza kuwasaidia kwa kuwasaini kwenye Lebo yake ili bado awe na nguvu ya kuwasapoti.

4 Kuongeza Timu ya washauri: Kingine Kiba anapaswa kuongeza idadi ya watu anaofanya nao kazi ambao ni official lakini hata kuwafanya nao wawe mastaa ili popote wanapofanya interview nado yeye atajwe mfano Alichofanya DÄ°AMOND amembrand DESÄ°GNER, DANCERS ,MAMA, MTOTO, DADA kote huko bado jina lake linatrend

#kijanamzalendo #ilovetz #maoniyangu