Ticker

10/recent/ticker-posts

Sababu 25 za Uhakika Kwanini ni rahisi Mwanamke Kumsaliti Mpenzi wake.?Soma hapa

Tokea kuumbwa kwa dunia, kidini na kihistoria, mwanamke amevunja rekodi kuwa kiumbe dhaifu na rahisi zaidi hasa katika nyanja ya usaliti, mtoto wa kiume uzaliwapo na ukafikisha umri wa barehe jambo na usia mkuu uambiwao na baba yako au kusikia tokea kwa wazee ni moja na linatiliwa sana mkazo "Usimwamini mwanamke".

 Leo kiumeni.com tumetilia mkazo kuangalia sababu halisi za maisha ya kweli zinazowafanya hawa viumbe kuwa hivi, sababu ya kwanini wanakuwa ni rahisi kwao kufikia huu uwamuzi na nini kinachowapelekea kuwa rahisi kuuwamua.

#1 Wanawake huwa na mazoea ya kumzoea mtu kwa haraka zaidi. Ni rahisi sana kwa mwanamke kutengeneza uhusiano wa kihisia na mtu mwingine kwa haraka, hii inawafanya kuwa rahisi kumzoea mwanaume na kudhania hayo mazoea aliyoyaanzisha ni mapenzi.

#2 Wanauwezo wa kupenda Mwanaume yoyote anaowaonyesha kuwajali na kuwapa msaada wa kihisia. Ni kweli, kama unataka umuibe mpenzi wa mtu muonyeshe kumjali na kumpa msaada wa kihisia, akiwa na siku mbaya jaribu kuitengeneza iwe nzuri na mpe misaada midogo midogo naye atakupa kitanda cha kulalia.

#3 Wanawake hupendelea kuendeleza kizazi. Kibaiolojia wameumbwa hivyo kuwa na hitajio la kuendeleza kizazi hivyo hujikuta wanaangalia wanaume wengine wenye sifa nzuri zaidi ya kutayarisha kizazi kijacho.

#4 Wanawake huanguka kimapenzi kwa urahisi zaidi. Huangukia kwenye mapenzi kwa uharaka zaidi kwa yule ambaye atawaonyesha hisia za kuwataka, wanaweza kuwa wanapenda kucheza michezo ya kukuzungusha ila mwisho wa siku hujikuta wanahisia flani juu yako iwapo ukiwa king'ang'anizi na mbwembwe za kimahaba, huku ukionyesha unaupendo wa dhati.

#5 Wanawake huwa ni wageuzi wa mambo. wanapenda wakiwa na mwanaume wambadili kwa jinsi wamtakavyo wao, wakisha mbadili wanaboreka na kuanza kutafuta mwingine, kwahio siku zote msichana asikubadilishe anavyokutaka yeye, akikubadilisha tu anaboreka, unakuwa haumpi akshi tena ya kukuona angavu kama awali na wewe na kutafuta mgumu mwingine wa kumfanyia mabadiliko, hakikisha asikuelewe na mshitukize kwa mambo ya hapa na pale kumpoteza zaidi.

#6 Wanawake wanapenda michezo ya kuigiza na umbea. Wanawake wanaboreka kirahisi sana na huitaji uwape kipaumbele muda wote, mwanaume anapoanza kumpenda kupitiliza, yeye ndo anaanza kutokua na hamu tena ya hayo mapenzi, ndo maana waswahili husema "usimuonyeshe mwanamke kama unampenda".

#7 Hawajielewi ni kipi hisia zao zinataka, na huwa hivi mara nyingi. Msichana anaweza kuwa anampenda mwanaume ila mabadiliko ya hisia zao kama kupwa na kupwaa kwa bahari akawa kama saa nyingine anampenda na muda mwingine akawa kama hana shida naye na kumponda, kwa hio ukiongeza mwanaume mwingine kwenye hio hadithi nadhani utakuwa unapata picha.

#8 Wanawake wanapenda kusifiwa na kuonyeshwa kupendwa. Wanawake hujisahau wakianza kusifiwa na kutongozwa kwa kuguswa. Mwanaume akianza kumtongoza mwanzo huhisia labda anamtania ila kwa uhalisia inawezekana akawa anaangukia kimapenzi kwa jamaa hata kama jamaa anatania.

#9 Ni rahisi sana kumfanya msichana awe na mashaka na mpenzi wake. Jamaa mwingine anachotakiwa kukifanya ni kumuonyesha mapungufu ya mpenzi wake, kuongea vizuri, kumshika sehemu chache, na hapo kutamfanya msichana aanze kufikilia mpenzi wake si lolote si chochote, na huyu jamaa alienae ni mungu wa mapenzi na anampenda kufa na kupona.

#10 Wanawake husema hawapendi kuharibika kifikra. Ila kiuhalisia kitu wanachokifikilia ni kitaka kupotelea kwenye starehe zote za kidunia, kila mara mwanamke anapotongozwa huwa hujisahau kuwa anampenzi tayari!

#11 Wanawake hufumba macho wakati wanambusu mwanaume mwingine.Ndio hivyo, fumba macho yako na iwapo ukiulizwa sema mambo yalitokea kwa uharaka sana, wanawake hujikuta wameshafanya mapenzi na mwanaume mwingine na kusema yalikuwa ni makosa amekosea tu au anaweza kung'ang'ania haijatokea na hauna kidhibiti unasikiliza maneno ya watu, ulishawahi kuona wapi watu wakaongelea kitu ambacho hakijatokea?

#12 Wanawake sikuzote huhisi wapo kwenye matatizo ya kimahusiano.Mahusiano ya mwanaume na mwanamke yakidolola na kutokuwa na hakshi za kimahaba mwanamke huhisia kuna tatizo la kimahusiano, hivyo mwingine akija akaonyesha akshi zaidi.. Mmmhn, hapo jibu unalo.

#13 Wanawake wote huhisi wao na bora sana kwa wapenzi wao. Haya maono sijui wanayapata wapi, utamsikia "Shukuru upo na mie, angekuwa msichana mwingine asingekuvumilia!". Kwa mwendo huu unadhani atashindwa kuharibiwa iwapo jamaa mwingine anaejua kujikweza akijipanga vizuri?

#14 Wanawake husaliti kwa sababu za kipuuzi zaidi. Wanaume husaliti wakimpata mwanamke anaetamanisha kimahaba, ila mwanamke husaliti kwa sababu ya kumkomoa mwanaume, au kumuonyeshea mwanaume, au kitu chochote kingine kujionyesha yeye bado binti wanaomtaka ni wengi.

#15 Wanawake wanamatamanio. Ambayo ni chokuleti na sifa nyingine ambazo mpenzi wake hana, kama mpenzi wake sio msafi, akija jamaa au mfanya mfanyakazi mwenzie ambaye ni mtanashati, atajikuta anaanza kuvutika nae kwa sababu ya usafi, kwa hio kama mwanaume anamtaka msichana wa mtu anachotakiwa kufanya ni kumsoma ni kipi jamaa yake ambacho hana na akitumie vizuri ndani ya siku chache atakuwa na huyo msichana kitandani.

#16 Wanawake huvutika kwa mwanaume ambae anawafanya wajisikie vizuri.Wanaume huvutika na wanawake wenye maumbile ya kimahaba, kwa hio kumpata mwanamke wanaomuota huwa ni kazi ila wanawake huvutika na mwanaume yoyote yule, hata mjinga mjinga anaejua kumfanya ajisikie vizuri kuliko anavyokuwa na mwanaume wake, mwanamke atajikuta amesharubuniwa kupelekwa kitandani.

#17 Mwanamke ni mpenda vitu. Kama mwanamke uliyenae ni mpenda vitu na raha unazompa, na hayupo kihisia na wewe basi jua ni muda tu kabla hajakusaliti.

#18 Wanawake hufanya usaliti hisia zao zikiwa katika mazingira magumu.Wanaume wanahitaji mwanamke mwenye umbo la mitego kufanya usaliti, ila wanawake wanahitaji kuhisi wapo katika mazigira magumu kihisia, na hujihisi wapo katika mazingira magumu kwa sababu ndogo ndogo na mazingira, jamaa mwingine akijipanga na kuongea maneno matamu katika wakati mzuri anaweza kumpata usiku huo huo.

#19 Wanawake walio na msimamo katika mapenzi hupenda pia kuangaliwa na wanaume wengine. Ikiwa mwanamke hapewi kipaumbele na mwanaume aliyenaye, hujisahau na kukuta wakiangalia kwingine ili ajione bado analipa.

#20 Wanawake huwa hawajfunzi kutokana na makosa. Wanawake wakifanya makosa hujutia ila huwa hawawezi kujifunza, huwa wanajua pale mwanaume mwingine anapovuka mstari ila huwa hawamkemei kwa sababu wanapenda kuona wanatakwa.

#21 Wanawake husaliti wakiwa hawafurahishwi kitandani. Je unamwaga mapema au unatatizo la kukurupuka bila kupangilia mashambulizi na kumuandaa mpenzi wako? Hii ni sababu tosha ya mwanamke kukusaliti.

#22 Mahaba ya mwanaume yanapopungua. kama wanamke hatokuwa anavutika na mwanaume wake tena, hio ni sababu tosha ya kumfanya atafute mahaba yanayomkosha kwingineko.

#23 Wanawake hutongozwa zaidi. Mwanamke hutongozwa na mamilioni ya wanaume kila sehemu anapokwenda, unahisi itamchukua mda gani mpaka shetani atakapomchukua na kufanya jambo ambalo badae atalijutia? Wanaume wengine ni wataalamu matata wa utongozaji na wanaijua vizuri kazi yao na jinsi ya kutoa vishawishi kwa viumbe hawa dhaifu.

#24 Mwanamke akisha fanya mara moja ndo mazoea. Mwanamke anaweza kusaliti na mwanaume wake asijue ila baada ya muda hujikuta kasaliti tena, wanawake wanahisia mbaya ya kuangukia mapenzi kwa vishawishi.

#25 Hivi wanawake kweli huwa wanahitaji kuwa na furaha? Mwanamke anaweza kuwa kwenye uhusiano mzuri wa muda mrefu ila akija kukutana na mwanaume mwiba wapenzi za watu hujikuta anaangukia kwenye vishawishi na kuangukia kwenye mapenzi ya nje. hujawahi kuona mwanamke kwenye familia mume anahela na uwezo mkubwa ila anachukuliwa na hausi boi?, wanawake huwa wanahitaji furaha ya muda na mvurugano wa mawazo kwa muda mwingine uliobaki.

Kama unajiuliza kwanini wanawake wanasaliti kwa wepesi nadhani ndani ya sababu 25 utakuwa umepata jibu lako.