Ticker

10/recent/ticker-posts

MISS JIHAN DIMACHANAOGOPA KUMTAJA MPENZI WAKE KWASABABU YA KIKI

jihan
Miss Universe 2016 na mshindi wa tatu wa Miss Tanzania 2014, Jihan Dimach amesema kwa sasa hayupo kwenye mahusiano ya mapenzi akidai kuogopa kuharibiwa malengo yake.

Akiongea na Bongo5 Jumamosi hii, Jihan amesema wasichana wengi wanaaribika kutokana na ‘kiki’ pamoja na mambo yakubadili wanaume kila mara wakiamini wanapata kiki.
“Mimi sio mtu wa ‘kiki’ na sipendagi skendo naona kama zinachafua career yangu kiukweli siwasemei wengine lakini kama unataka kuendelea na career hii lazima ukae mbali na mambo hayo,” alisema Jihan. “kusema kweli sipo kwenye mahusiano am really focused on my caree kwa sasa,”
Jihan amesema anaamini ili afanikiwe ni lazima afanye kwanza kitu kilichomsimamisha kwenye mitindo ndipo baadae afanya mambo mengine.
Mrembo huyo anatarajia kuiwakilisha Tanzania katika mashindano makubwa ya urembo duniani Miss Universe ambayo yatafanyika mapema kwakani.

SHARE