Ticker

10/recent/ticker-posts

MENEJA SALLAM SK ATOLEA UFAFANUZI UJIO WA PERFUME YA DIAMOND


Usiku wa jana katika mtandao wa Instagram DIamond Platnumz alipost video ikionyesha perfume yake mpya ambayo inatarajiwa kuingia sokoni hivi punde ambayo inaitwa Chibu Perfume.
Perfect255 imeona sio kesi kama ikimtafuta meneja wa mkali huyo Sallam SK na kupiga nae story ili kutolea ufafanuzi brand hiyo mpya ambayo inatarajiwa kumuingiza Diamond Platnumz katika list ya wasanii wachache duniani ambao ni wajasiriamali na wanaoingiza mkwanja mrefu sana tofauti na kazi ya muziki.
Sallam amefunguka mengi sana juu ya perfume hiyo ikiwemo sababu ya wao kuiita perfume hiyo Chibu na sio Diamond kama lilivyo jina lake. Amedai kuwa jina la Diamond limeshakuwa kubwa sana na huu ndio wakati muafaka wa kubrand vitu vingine na kuvifanya vikubwa.
Sallam ametolea mfano kwa mastaa wakubwa duniani kama P Didy na kudai kuwa wao wana majina makubwa ndio maana hata bidhaa zao hajaamua kuzipa majina yao.
Play hii video hapa chini kumsikiliza Sallam akifunguka kiufafanuzi zaidi juu ya suala hilo.