Ticker

10/recent/ticker-posts

MAPENZI:Mwanaume Fanya Hivi ili Mkeo Akuone Mtenda Miujiza Kila Siku..Hakika Hatasikia la Mtu...



Hili ni fundisho kwa vijana wengi ambao wanataabika, suala la fedha limekuwa mwiba mkubwa na chanzo kikubwa cha mahusiano na ndoa kuyumba. Nimelazimika nije na ushauri huu ambao utawasaidia vijana wa kileo ambao wanataabika na ndoa hususani suala la fedha.

Kinachowaumiza vijana wengi katika fedha na wenza wao ni tabia ya wanaume kuwa wazi kwa kutoa taarifa za pato lake kamili. Jambo la uwazi ni jema lakini muwe na kiasi kwani usipokuwa na akiba ya 'taarifa za kipato chako' utakosa fusra ya kufanya miujiza pale mambo yanapokwama.

Fanya hivi. Mfano kipato chako ni shilingi milioni moja kwa mwezi, mweleze kwamba unapokea shilingi laki 7 na hizo tatu hakikisha unaweka katika sehemu salama ambayo hata ikitokea umekufa familia yako itafaidika, mfano benki kila unapochukua mshahara hakikisha unaacha laki tatu kama akiba asiyoijua. Sasa katika hii laki saba panga matumizi pamoja na akiba ya pamoja.

Wanawake wanapenda 'mshtuko/suprise'..so siku ya siku ukiona kanuna unamtoa shoping lazima ataona umetenda muujiza kwa nia njema. Hapa ndipo pale utasikia mwanamke anasema 'mme wangu ana akili kweli'. Ikitokea una marupurupu fulani kama safari nk hakikisha unatoa kiasi na ziada unaweka chimbo. Hii itakupa upenyo wa kuwasaidia hata wazazi wako na ndugu zako bila kumhusisha mara kwa mara kwani wanawake wengine hawapendi usaidie ndugu na jamaa. Fanya mbinu hii hata kama kipato chako ni laki tano weka hata elfu hamsini chimbo ili uweze kutenda baadhi ya miujiza.

Wanawake wote duniani wamejaliwa karama ya kutumia hela yote ya mmewe, yaani ukimwambia kuna hela hii yeye ataandika orodha ya mahitaji ya familia ni kwani njema ila pesa zikiisha yeye hujitoa na kukulaumu kwanini ulitumia pesa zote. Yaani dharura ikitokea yeye hayupo ni lako hilo na ukishindwa kutatua hapo ndipo dharau inaanza...utasikia 'mme wangu hana msaada kabisa' yaani hajali kabisa matatizo anatumia pesa zote bila uangalifu.

Haya yote yanahitaji ustadi mkubwa na utimamu, kumbuka siku zote mwanaume anatakiwa kuwa mtu wa mshitukizo/surprise kwa kutumia kipato kile kile alichonacho. Yaani tunasema uwe na uwezo wa kutengeneza hela (money creator). Ikitokea dharura unamuangalia usoni huku ukitabasamu, unamwambia 'mke wangu usihuzunike ngoja nifanye mpango nitatue hii shida'.

Hii ndio mbinu tuliitumia sisi na kuweza kuishi na mama/bibi zenu bila bugdha.

Nawakilisha.