Ticker

10/recent/ticker-posts

DOGO JANJA AFUNGUKA MAHUSIANO YAKE YA KIMAPENZI NA AGNESS MASOGANGE




U Heard ya XXL Clouds FM leo November 2, 2016 Soudy Brown amemvutia waya staa wa single ya Kidebe, Dogo Janja ambaye inadaiwa yuko kwenye uhusiano wa kimapenzi na staa mwingine wa kike Agness Masogange.
Dogo Janja amesema kuwa picha inayoonekana kwenye mitandao watu wameitafsiri tofauti tu wao walikua sehemu moja ila mpiga picha alipigia sehemu ambayo iliwaonyesha kama wako chumbani huku Dogo Janja akiangalia sehemu za nyuma za Agness.
“Masogange ni mshikaji wangu sana ni mtu wangu wa karibu watu wamezoea kuniona na marafiki wa kiume tu ni rafiki yangu na niko kwenye maongezi naye kuhusu kushoot video’ – Dogo Janja
"Unajua baada ya Kidebe nafikiria jinsi ya kurudi tena na wimbo wangu mpya, ukitoa mambo ya kikazi yule ni mshikaji wangu, Agness pale alikua amekaa tu sio kwamba alikua ananionesha makalio ila nisipomtamani yule nitakua na matatizo" – Dogo Janja

Kusikiliza full story bonyeza play hapa chini.