Ticker

10/recent/ticker-posts

CYRIL NA SIRI YA KUSHOBOKEWA NA WAREMBO

MWANAMUZIKI mkali wa Bongo Fleva, Cyril Kamikaze ‘Sindgida Boy’ amefungukia ishu ya kushobokewa na mastaa warembo akisema kuwa inamtokea sana lakini anawapotezea kiasi cha kupachikwa jina la ‘Chamajidai’ Akichonga na Cyril alisema kuwa, tangu amekuwa staa wapo warembo wengi wanaomtaka kimapenzi lakini kwa kuwa ana msimamo wake, huwatolea nje hali inayosababisha wamchukie na kumuona anaringa. “Mimi kwa kweli mrembo akiniambia ananipenda najiuliza mara mbili mbili kivipi? Hii ni kwa sababu najua wazi anataka kuniumiza maana tukishakuwa wapenzi baada ya muda tutakorofisha, tutaachana. Huwa nawapotezea tu, acha waniite majina wanayojisikia, mi’ sijali,” alisema Cyril.