Ticker

10/recent/ticker-posts

BAADA YA SERENGETI BOY KUJINADI KULIFAIDI KUFAIDI PENZI LAKE, WOLPER ACHUKULIA KAMA CHANGAMOTO!

Mrembo na staa wa bongo movies, Jackline  Massawe Wolper ameonyesha kuchukulia ni kama changamoto kitendo cha msanii wa muziki kutoka kundi la makomando Fredy Felix  ambae ni bwa’mdogo “Serengeti Boy” kujinadi hadharani kuwa alikuwa na mahusiano ya kimapenzi na Wolper huku akielezea njinsi alivyompata na kumsifu kuwa alimpata penzi ambalo hatoweza kulisahau.

Felix aliyasema hayo hivi juzi kati alipokuwa akifanya mahojiano na Global Tv online nakusababisha stori hii kuenea kwa kasi sana kwenye magazeti na blogs za udaku.

Leo kupitia ukurasa wake wa Instagram Wolper aliandika ujumbe unaoonyesha  kwa namna moja au nyingine kitendo hicho amekichukulia kama ni changamoto tu za maisha ya zamani.

Wolper aliandika maneno haya kwa lugha ya kimombo

“The past can hurt but the way I see it, you can either run from it or learn from it”.

Kwa tafsiri isiyo rasmi anaamanisha kuwa mambo yaliyopita yanaweka kuumiza lakini kwa jinsi anavyo yatazama yeye , unaeza kuyakimbia au kujifunza kutokana yaliyopita.

Mara baada ya ujumbe huu, mashabiki wake wengi walimpa moyo huku wakimponda kijana Felix kwa kufanya kitendo ambacho wengi walisema cha kipumbavu.