Mastaa wakubwa Afrika Mashariki, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ na Zarinah Hassan ‘Zari’wakila ujana.
Acha
muvi iendelee! Ile projekti ya mastaa wakubwa Afrika Mashariki, Nasibu
Abdul ‘Diamond Platnumz’ na Zarinah Hassan ‘Zari’ sasa imenoga.
Habari zinaeleza kwamba katika pati ya mwaka ya Zari wiki iliyopita
iliyofanyika kwenye Ukumbi wa Guvnor uliopo Kampala, Uganda mwanadada
huyo hakuishia kwenye pati tu bali alitumia nafasi hiyo kumtambulisha
Diamond aliyekuwa mgeni rasmi kuwa kwa sasa wao ni wapenzi.
‘Diamond Platnumz’ na Zarinah Hassan ‘Zari’ wakifanya yao.
Mbali na
mahaba niue waliyooneshana mbele za watu, wawili hao walitumia chansi
hiyo ‘kudendeka’ mbele ya kamera hivyo kudhihirisha kwamba mambo yao
yapo juu ya mstari.