Ticker

10/recent/ticker-posts

MASTAA WEMA NA PENNY KUFANYA MOVIE PAMOJA SASA..!!ITAKUWA NI SHEEDAH

 
Walikuwa marafiki wa damu, wakaja kuwa maadui.. na sasa ni marafiki tena. Baada ya kupatanishwa kwenye sherehe ya kuzaliwa ya Junaithar siku kadhaa zilizopita, Wema Sepetu na Penny Mungilwa wameendelea kuuimarisha zaidi urafiki wao.
Penny ameshare picha kwenye Instagram akiwa pamoja na Miss Tanzania huyo wa zamani ambayo Wema pia ameirepost kwenye akaunti yake. Hiyo ni picha ya kwanza ya warembo hao wakiwa pamoja kuwahi kuweka kwenye akaunti zao katika kipindi kirefu.

Wakiongea kwa pamoja na Bongo5 leo wakifanya shopping ya nguo, warembo hao wamedai kuwa wana mipango ya kufanya filamu pamoja na wanatarajia kuingia kambini mwakani.

Picha hiyo imepokelewa kwa furaha kubwa na mashabiki wao wanaopenda kuwaona wakiwa pamoja.