Muigizaji wa the "Expendables
3" Sylvester Stallone amekuwa mmoja wa mastaa wa Hollywood ambao
wamekuwa ni waathirika wa kuzushiwa kifo. Tetesi zilizosambaa kama moto
unaounguza pori/ msitu hasa hasa kupitia mitandao ya kijamii, zilianzia
kupitia ukurasa feki wa facebook.
Habari
hii ambayo inaonekana kusababisha panic kubwa kwa mashabiki wa
muigizaji "Rambo" imepelekea kutumwa kwa salamu za huzuni kutoka kwa
mashabiki wake mbalimbali kupitia mtandao wa twitter.
Ripoti hizo za
kifo cha Rambo zinadai kuwa alipata ajali mbaya ya gari iliyosababishwa
na dereva wake aliekuwa amelewa na kutokuona gari kubwa lililokuwa
likija mbele yake.
Hii
sio maara ya kwanza kwa muigizaji huyo kuuliwa na internet, mwanzoni
uvumi mkubwa wa kifo chake ulioripotiwa na Global Associate News zilidai
kuwa Rambo alifariki kwa ajali iliyotokana na snowboarding.
0 Comments