Hatimaye! Kwa mara ya kwanza staa ‘the big name’ wa Bongo Fleva ndani na nje ya Bongo, Ali Saleh Kiba ameibuka na kumlipua hasimu wake, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, hali inayotafsiriwa kwamba bifu lao sasa limefika pabaya ikidaiwa kwamba wanagombea nyota (ustaa).
Kupitia Kipindi cha The Sporah Show,
usiku wa Jumanne wiki hii kwenye CloudsTV, Kiba alimchakaza Diamond
ambapo alifunguka mengi ikiwemo chanzo cha ugomvi wao.
Kiba
alizungumzia sosi iliyotengeneza bifu kati yake na Diamond ambapo
aliulizwa kama ana namba ya simu ya msanii huyo ndipo akatiririka:
“Nilikuwa nayo kipindi fulani, nilipohisi amenikosea nikaona sina ulazima wa kuwa nayo.
“Kuna
kipindi alinikosea kwa sababu nilisikia amesema kwamba tulirekodi wote
ule Wimbo wa Single Boy, jambo ambalo halikuwa kweli. Halafu akasema
mimi ndiyo nilimfuta.
“Diamond alinikosea kwa sababu kutokana
na mimi ndiye nilifanya wimbo wake wa Lala Salama ambao upo kwenye
album yake, akanifuta nikahisi amenikosea sana nilichoimba mimi akawa
ameimba yeye, alichoniomba nifanye nilifanya kwa mapenzi yote na mimi
namsapoti kila msanii wa Tanzania anayefanya vizuri, sikatai anaimba
vizuri, sijui ukisema amekopi, mimi sijamaindi wala nini lakini usiseme
kwa watu ukadanganya nikaonekana mimi sifai, siko hivyo mimi.
“Watu wengine ambao hawaelewi vizuri
wanaweza wakamwamini Diamond, kila mtu ana mapenzi yake labda kuna
wengine wanampenda Diamond wengine wanampenda Ali Kiba. Wanaweza wakawa
wengine wanampenda Diamond wakaamini mimi nilimfuta kwenye wimbo wangu
wa Single Boy lakini mimi wala, shahidi yangu ni produyuza Manecky (AM
Records) kwani ndiye alitengeneza ule wimbo.
“Sikuwahi kwenda studio na Diamond,
sikuwahi kufikiria kufanya wimbo naye. Ila alinipigia simu baada ya ule
wimbo wa Single Boy kuvuja. Akaomba afanye na mimi, akanipa hadi idea
(wazo) ya video, nikamwambia nimeshafanya na Jaydee (Judith Wambura).
Nikamwambia itapendeza zaidi tukifanya
wimbo mwingine kwa sababu hii tukifanya mimi na wewe haita-make sense
(haitaeleweka), inapendeza ikiwa single boy na single girl, hicho ndicho
kitu nilimjibu.
“Baada ya
kama wiki moja nikasikia kwenye mablog, nikapigiwa simu kwamba mimi
nimemfuta Diamond kwenye ule wimbo wakati yeye ndiye aliyenifuta katika
wimbo wake, shahidi prodyuza wangu KGT.
“Kutoka
hapo nikaona hakuna tatizo lakini kwa kujua yeye alinifuta katika wimbo
wake. Mimi siyo shabiki wa Diamond ni shabiki wa muziki mzuri. “Kuna
watu wanasema kachukua kiti changu? Labda kama ni kiti ambacho nilikuwa
nimekaa kina vumbi na ninachotakiwa ni kukipangusa tu na kukaa tena,
labda yeye yuko siti nyingine ila ya nyuma.
“Niliambiwa alisema vitu vingi, mara
nilikopa fedha benki ili nimalizie nyumba na mambo kama hayo so siwezi
kufanya naye kazi.” Baada ya Kiba kumchakaza, kupitia ukurasa wake wa
Instagram, Diamond naye alijibu mapigo bila kutaja jina la Kiba ambapo
aliandika: “Tatizo lako wewe unawaza kushindana na mimi ili
nishuke…Wakati mwenzako nawaza kushindana na watu wa mataifa mengine ili
nilete sifa na heshima nchini kwetu.”
Hata hivyo, baada ya hayo yote
kuliibuka madai kwamba mbali na ishu za muziki, mastaa wa kike wa sinema
za Kibongo, Jacqueline Wolper Massawe, Elizabeth Michael ‘Lulu’ na Wema
Isaac Sepetu wanahusishwa kwenye gogoro hilo kisa wivu wa kimapenzi
hivyo ishu hiyo bado ni mbichi. Tusubiri mwisho WAKE
0 Comments